Lionel Messi amefikia rekodi ya
magoli 251 iliyowekwa na Telmo Zarra, kwa kufunga goli tamu la mpira
wa adhabu, baada ya kushindwa kufunga katika michezo mitatu iliyopita
ya La Liga.
Katika mchezo huo na Sevilla
ilisawazisha bao hilo kupitia goli la kujifunga la Jordi Alba, kabla
ya Neymar kuifungia Barcelona bao la pili.
Nae Ivan Rakitic naye alifunga bao
lake kwa kichwa, kabla ya Messi kucheka tena na wavu na kuweka rekodi
mpya ya magoli 253 kufuatia gonga baina yake na Mbrazil Neymar na
hadi mwisho Barcelona 5 Sevilla 1.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni