Makamu wa Rais Joice kushoto akiwa na rais Robert Mugabe
Makamu wa rais wa Zimbabwe
ameng'olewa madaraka katika chama tawala, kufuatia kampeni
iliyofanywa na mke wa Rais Robert Mugabe, Grace huku kukiwa na
mvutano wa nani atamrithi Mugabe ukipamba moto.
Makamu huyo Joice Mujuru amejikuta
akishambuliwa na Grace Mugabe, aliyedai kuwa makamu huyo wa rais
anachukua fedha kwenye kampuni na kuunda makundi yanayotishia
kukipasua chama tawala cha ZANU-PF.
Bi. Mujuru anatuhumiwa kupanga njama
za kumuua rais Mugabe, wakati watu katika chama hicho wakipambana
kutafuta kurithi nafasi ya urais pindi atakapoondoka madarakani rais
Mugabe mwenye umri wa miaka 90 ama atakapofariki.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni