.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 27 Novemba 2014

MCHEZAJI WA KRIKETI WA AUSTRALIA ALIYEPIGWA NA MPIRA KICHWANI AFARIKI DUNIA

Mchezaji kriketi wa Australia Phil Hughes amefariki dunia hospitali ikiwa imepita siku mbili baada ya kupigwa kichwani na mpira wakati wa mchezo uliofanyika Sydney.

Mkuu wa Timu ya Madaktari wa Australia, Dk. Peter Brukner amesema mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25, hakurejewa na fahamu tangu apatwe na tukio hilo.

Hughes, ambaye pia alichezea timu za Hampshire, Middlesex pamoja na Worcestershire, alipigwa kichwani na mpira wa karibu uliopigwa na Sean Abbott. 
                           Tukio lenyewe lilikuwa hivi..hapa mpira ukimpiga kichwani
                           Phil Hughes akianguka chini baada ya kupigwa na mpira huo
Bowler Sean Abbott aliyempiga na mpira Hughes akitoka hospitali akiwa na huzuni baada ya kupewa habari ya kifo.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni