Wandesha mashtaka nchini Nigeria
wamemfungulia kesi mtoto wa kike wa miaka 14, kwa tuhuma za kumuua
mumewe mwenye umri wa miaka 35.
Katika kesi hiyo mtoto huyo Wasila
Tasi'u anadaiwa kununua sumu ya panya na kumuwekea kwenye chakula
mumewe na kumsababishia kifo.
Mtoto Tasi'u anayetokea familia
masikini katika eneo la Kaskazini, anaweza akahukumiwa kifo iwapo
atatiwa hatiani, ambapo wanaharakati wa haki za watoto wa kike
wakisema mtoto huyo hapaswi kutiwa hatiani.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni