
Majaribio ya kwanza ya chanjo ya
Ebola kwa binadamu, yameonyesha kuwa ni salama na yanaweza kuimarisha
kinga dhidi ya virusi vya ugonjwa huo.
Watu 20 wamepatiwa chanjo hiyo baada
ya kujitolea katika nchi ya Marekani, na wanasayansi wa Taasisi ya
Taifa ya Afya ya nchi hiyo, wamesema matokeo yake yanaleta matumaini.
Matokeo ya utafiti huo yanaonyesha
hakuna mtu yeyote aliyechanjwa aliyepata madhara, bali kinga yao
imeimarika.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni