Waziri wa Afya nchini Hispania Ana
Mato amejiuzulu baada ya jaji kumtuhumu kunufaika na malipo fedha
haramu.
Aliye kuwa mumewe Jesus Sepulveda
amebainika kuhusika na kashfa kubwa ya rushwa katika kesi
inayohusisha chama tawala cha Peoples.
Mahakama imetoa uamuzi unaoonyesha
Bi. Mato hakuwa na ufahamu wa kutokea kwa uhalifu wowote ule.
Kesi hiyo ilipelekea Waziri Mkuu
Mariano Rajoy, kuguswa na kashfa hiyo na kuomba msahmaha baada ya
wanachama wa chama chake kukamatwa na polisi.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni