Wakazi wa eneo la Majengo Mombasa
Kenya sasa wanaweza kuingia kwenye misikiti iliyofungwa, baada ya
makubaliano baina ya serikali, wanataaluma na viongozi wa Kiislamu ya
kufunguliwa kwa misikiti hiyo.
Kumekuwepo na ulinzi mkali katika
mji huo wakati msikiti wa Masjid Musa ulipofunguliwa mapema leo.
Makumi ya watu walikusanyika
kushuhudiwa kufunguliwa kwa msikiti huo wakati vijana wakichukua
majukumu ya kuusafisha msikiti huo pamoja na mazingira yake.
Misikiti mingine ya Sakina, Minaa na
Swafaa nayo pia ilikuwa inatarajiwa kufunguliwa hii leo.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni