Vitendo vya ukatili wa kutisha vya
kuwatoa kafara watoto vikihusisha kuwakata viungo vyao na kupelekea
vifo watoto vimezidi kushika kasi nchini Uganda.
Kwa mujibu wa ripoti ya mwaka 2013
ya watoto waliotolewa kafara na kukatwa viungo Uganda inaonyesha
kumekuwa na kitendo kimoja cha kumtoa kafara mtoto kila wiki,
ikilinganishwa matukio saba ya kuwatoa kafara watoto yaliyoripotiwa
polisi katika mwaka 2011.
Utoaji kafara watoto hao unahusishwa
na masuala ya kiuchumi na mila za Uganda na hufanywa maganga wa
kienyeji, mawakala wao na wateja kwa iamani viungo vyao ni dawa yenye
nguvu inayotibu magonjwa yote na kutoa ufumbuzi wa matatizo mengi.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni