Makundi ya watu yameandamana katika
maeneo mbalimbali nchini Marekani kupinga uamuzi wa mahakama
kutomfungulia mashtaka afisa polisi aliyemuua kijana mweusi Michael
Brown kwa kumpiga risasi.
Maandamano kuanzia Jijini New York
hadi Seattle yalikuwa ya amani, huku waandamanaji wakipaza sauti zao
na kupeperusha mabango yenye ujumbe mbalimbali.
Katika kitongoji cha St Louis eneo
la Ferguson, ambapo vurugu zilitawala siku ya jumatatu, jumla ya
askari polisi 22,000 wamesambwazwa katika kudhibiti kutokea machafuko
makubwa zaidi.


Hakuna maoni :
Chapisha Maoni