Serikali ya Kenya imekataa kuwaondoa
makumi ya maafisa wa umma pamoja na familia zao walioweka kambi
katika uwanja wa ndege wa jeshi, wakiwa na mali zao baada ya kutokea
tukio la kuuwawa wenzao 28 na kundi la al-Shabaab siku ya jumamosi
huko Mandera.
Badala yake serikali ya Kenya,
imewataka wafanyakazi hao kurejea kazini, na kuwahakikishia kuwa
usalama wao utalindwa.
Hata hivyo watumishi hao wa umma
wameendelea kushikilia msimamo wake kuwa wanahofia usalama wa maisha
yao na kamwe hawataondoka katika eneo hilo la jeshi.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni