Watumishi wa kuzika maiti mashariki
mwa Sierra Leone wamefukuzwa kazi baada ya kupora miili ya watu
waliokufa kwa Ebola katika chumba cha maiti, na kuitupa maiti zake
kwenye barabara kutokana na mgogoro wa malipo yao.
Watumishi hao waliokuwa katika mgomo
wa siku moja kudai kutolipwa posho za kufanyakazi katika mazingira
hatarishi, walitawanya makumi ya miili hiyo kuzunguka hospitali
katika Mji wa Kenema.
Maiti za watu waliokufa kwa Ebola
pia ziliachwa mbele ya ofisi ya meneja wa hospitali hiyo kwa mujibu
maafisa wa hospitali hiyo ingawa haikuelezwa ni kwa muda gani miili
hiyo iliachwa ikitapakaa kwenye hospitali hiyo.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni