Hoteli nchini Saudi Arabia
zimewapiga marufuku wanawake wasioolewa kuingia hotelini kutokana na
tabia zao za kujigonga kwa wanaume, kuvuta sigara na kutumia muda
mwingi katika simu zao za mkononi.
Hoteli kadhaa zimeweka ubao
unaosomeka 'Wanawake Hawaruhusiwi', jambo ambalo ni pigo kwa watetezi
wa haki za binadamu dhidi ya utawala wa nchi hiyo wa Kifalme wa
Kiislam.
Hakuna sheria inayowakataza wanawake
kusafiri wenyewe nchini Saudi Arabia lakini kunaimani za ndani za
kidini kuwa wanawake wanapaswa kusindikizwa na mwanaume wa familia
anayotoka wawapo maeneo ya umma.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni