Watu wamekuwa wakidundana ngumi
katika baadhi ya maduka makubwa ya bidhaa nchini Uingereza, huku moja
ya tovuti kubwa ya kuuza bidhaa seva yake ikishindwa kufanya kazi,
wakati wateja wakihaha kununua bidha kwa bei chee kupitia ofa
ijulikanayo kama Black Friday.
Tovuti hiyo inayouza bidhaa za
maduka makubwa kama ya Boots, Game, Currys, Argos pamoja na Tesco
Direct imepata hitilafu leo asubuhi wakati wanunuzi walipoingia kwa
wingi kununua bidhaa online, ambapo bidhaa kama TV bapa, mashine ya
kahawa, nguo, fenicha, nguo, midoli pamoja na bidhaa nyingine za
nyumbani ziligombewa.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni