Imeelezwa kuwa watu wenye silaha
walifyatua risasi hewani hovyo kwa furaha baada ya kuwauwa watu 28
nchini Kenya ambao inasaidikiwa si waislam katika shambulio
lililotokea jana Arabiya eneo la Mandera katika mpaka wa Kenya na
Somalia.
Mmoja wa abiria aliyekuwemo kwenye
basi lililoshambuliwa na wapiganaji hao wanaosaidikiwa ni wa kundi la
al Shabaab, amesema watu hao waliokuwa wamefunika nyuso zao
walifyatua risasi hizo wakiwa a sialaha nzito kama G3 na AK47, vile
vile walitumia SMG na bastola.
Abiria huyo ambaye hakutaka kutaja
jina lake kwa sababu za kiusalama amesema wavamizi hao walikuwa
wanaongea lugha za Kiswahili, Kingereza pamoja na Kisomali, na
walikuwa wamevalia mavazi ya kijeshi.
Amesema kuwa walipofika eneo la
Arabiya, wavamizi hao wapatao sita wakiwa wameshehena silaha
walilisimamisha basi hilo, huku mmoja wao akiwa na kombora la roketi,
ambapo walifyatua risasi upande wa kushoto mwa basi kabla ya kuingia
ndani na kutekeleza unyama huo.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni