
Akiwasilisha mapendekezo hayo mbele ya waziri mwenye dhamana na Mazingira Mwenyekiti wa bodi ya Forum CC Euster Kibona amesema serikali inapaswa kubainisha mapendekezo ya kupunguza makali ya uharibifu wa mazingira kwa nchi zilizoendelea. Pia nchi zilizoendelea zikubali kuwepo na makubaliano ya kisheria na kuheshimu kanuni juu ya masuala yote ya mazingira.
Kibona ametoa wito kwa viongozi wa dunia na Afrika kuwashirikisha wadau wengine katika mchakato wa mikataba ya kimataifa ili kupunguza manung’uniko ya kutoshirikishwa kwa wadau. Pia amesema nchi zilizoendelea zinapaswa kutoa fedha ,teknolojia na kujenga uwezo juu ya kukabiliana na janga la uharibifu wa mazingira.


Hakuna maoni :
Chapisha Maoni