.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumanne, 2 Desemba 2014

JENERALI WA JESHI LA COLOMBIA ALIYETEKWA RUBEN DARIO ALZATE AJIUZULU

                                    Jenerali Alzate akiwa amezungukwa na familia yake
 
Jenerali wa Jeshi la Colombia Ruben Dario Alzate, aliyeachiwa huru na waasi wa FARC siku ya jumapili amejiuzulu wadhifa wake jeshini.

Jenerali Alzate akiwa na ulinzi mdogo alitekwa akiwa anasafiri kwa boti kwenye ukanda wa misitu eneo la kando ya nchi hiyo wiki mbili zilizopita.

Rais wa Colombia Juan Manuel Santos ametaka kupatiwa maelezo kutoka jeshini juu ya inawezekana vipi jenerali wa jeshi akatekwa na waasi.

Jenerali Alzate amekiri kuwa alikiuka kanuni za kuzingatia usalama wake wakati akikatiza na boti katika eneo alilotekwa.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni