Wachimbaji kokoto wapatao 36
wameuwawa hii leo nchini Kenya na wapiganaji wa kundi la Al-Shabaab
katika shambulio lililofanyika eneo la Koromei katika kaunti ya
Mandera.
Wachimba kokoto hao walishambuliwa
wakiwa wamelala kwenye hema na kuuwawa kwa kupigwa risasi na
wapiganaji hao.
Jeshi la polisi Kenya limethibitisha
kutokea vifo hivyo na kuongeza kuwa hawajabaini chanzo cha mauaji
hayo, ambayo yamewalenga wachimbaji kokoto wakristo tu.
Shambulio hilo limekuja saa chache
tu kupita tangu kundi moja kufanya shambulio kwenye klabu moja huko
Wajir na kumuua mtu mmoja na wengine 13 kujeruhiwa.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni