Lionel Messi ( mbele )
Manuel Neuer.
Hatimaye Shirikisho la kandanda ulimwenguni ( Fifa ) limetangaza majina matatu ya wachezaji ambao watawania tuzo ya Ballon d'Or kwa mwaka 2014/2015.
Katika majina hayo, yupo mshambuliaji mahiri wa timu ya soka ya Real Madrid na timu ya taifa ya Ureno, Cristiano Ronaldo ambaye aliitwaa tuzo hiyo mwaka jana.
Ronaldo atapambana na mshambuliaji hatari wa FC Barcelona na timu ya taifa ya Argentina, Lionel Messi.
Pia mlinda mlango mahiri wa timu ya Bayern Munich na timu ya taifa ya Ujerumani, Manuel Neuer ameingia katika hatua hiyo ya fainali ya kuwania tuzo hiyo ambayo itatolewa January 12' 2015 mjini Zurich, Uswisi.
Tujikumbushe waliopata kutwaa tuzo hii miaka iliyopita:-
2013 - Cristiano Ronaldo
2012 - Lionel Messi
2011 - Lionel Messi
2010 - Lionel Messi
2009 - Lionel Messi
2008 - Cristiano Ronaldo
2007 - Kaka
2006 - Fabio Cannavaro
2005 - Ronaldinho
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni