Kocha wa Manchester United, Louis
van Gaal amekishutumu kikosi chake kwa kukosa hisia za mauaji
zitakazowawezesha kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya Uingereza, baada ya
kulazimishwa sare ya bao moja kwa moja na Aston Villa.
Mchezaji Radamel Falcao alianza
katika mchezo huo tangu aichezee Manchester United mapema mwezi
Oktoba, na aliweza kupachika bao wavuni katika kipindi cha pili na
kuisaidia United kusawazisha bao, baada ya kuwa nyuma kufuatia bao la
Christian Benteke.
Manchester United iliyokuwa na
rekodi ya kushinda mfululizo mechi zake sita za nyuma, ilishindwa
kupata ushindi hata pale mchezaji wa Aston Villa, Gabriel Agbonlahor,
alipotolewa nje kwa kadi nyekundu katika dakika ya 65.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni