Mali zenye thamani ya maelfu ya
shilingi za Kenya, imeteketea kwa moto leo asubuhi kufuatia soko la
Nyayo lililopo Ngara Jijini Nairobi kuungua moto.
Badhi ya wafanyabiashara wachache
walimudu kuokoa mali zao kabla ya kuteketezwa na ndimi za moto huo
mkubwa.
Vikosi vya zimamoto vilishindwa
kudhibiti moto huo uliochochewa na mbao zilizojenga mabanda ya soko
hilo la nguo za mitumba.
Afisa mmoja wa polisi ambaye
hakutaka kutaja jina lake, amesema bado haijajulikana chanzo cha
kutokea moto huo.
Moto mkubwa ukiteketeza mabanda ya mitumba katika soko la Nyayo
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni