Mwanaume mmoja mwenye silaha
amewapiga risasi na kuwauwa maafisa polisi wawili, walikokuwa kwenye
gari la doria Jijini New York nchini Marekani, kabla na yeye kujiua
pia.
Mkuu wa Polisi Jijini New York
amesema mwanaume huyo alinuia kuua polisi, na baada ya kufanya hivyo
alikimbilia kwenye njia ya reli ya aridhini na kisha kujipiga risasi.
Mapema mwanaume huyo alimpiga risasi
na kumjeruhi mpenzi wake wa zamani, na kisha kutuma ujumbe wa chuki
dhidi ya polisi kwenye mitandao ya jamii.
Rais Barack Obama, ambaye yupo
katika mapumziko ya Sikukuu huko Hawaii, amelaani mauaji ya polisi
hao.
Silaha iliyotumika kuwauwa polisi
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni