Manchester City imeibuka na ushindi mkubwa dhidi ya wenyeji wao Sunderland wa mabao 41 katika mchezo wa ligi kuu nchini Uingereza ambao umechezwa usiku wa kuamkia leo.
Ikcheza ugenini, mabingwa hao watetezi wa kombe la ligi kuu nchini Uingereza walijipatia mabao yao kupitia kwa mshambuliaji mwenye uwezo mkubwa uwanjani Sergio Aguero ambaye aliifungia timu yake mabao mawili katika dakika za 21 na 71.
Bao la pili la Manchester City lilifungwa na Stevan Jovetic katika dakika ya 39 na bao la tatu likawekwa kimiani na Pablo Zabaleta 55.
Hata hivyo katika mchezo huo, wenyeji Sunderland ndio waliotangulia kupata bao katika dakika ya 19 ya mchezo mfungaji akiwa ni Connor Wickham.
Kwa matokeo hayo Manchester City wamefikisha pointi 30 wakiwa nafasi ya pili nyuma ya Chelsea.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni
(
Atom
)
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni