.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 4 Desemba 2014

NSSF YAJITOSA KUTATUA KERO ZA WAVUVI NCHINI.


Aidha Mashinga aliwasihii sana wana Ihale kuweza kutumia nafasi hii ya kipekee kwao, hivyo aliwaambia mara baada ya kumalizana na wavuvi watahamia katika sekta nyingine na lengo likiwa ni kuwakwamua katika janga la umasikini.

Kwa upande wake Afisa uvuvi wa wilaya hiyo ya busega Bi Judith Mgaya ameweza kutoa wito kwa wavuvi kuweza kujitokeza kwa wingi ili waweze kupata huduma ya hifadhi ya mfuko wa jamii kwani ni fursa ya pekee kwao kuweza kujikwamua katika hali ya uchumi hapa nchi pia Bi mgaya aliweza kutoa pongezi kwa shirika la Nssf kwa kutambua shida za wavuvi nchini na kuweza kupambana nazo.

Upande wa wananchi wa Ihali waliojitokeza kwa wingi kuweza kujiunga na huduma hizo za kijamii wakisemewa na Bw, Dionis Kabati anasema kuwa wao kama wavuvi wanaishukuru Nssf kwa kuweza kutambua kero zao na hata kupata elimu ya kuwa kuna mambo kama hayo ambayo sisi tulikuwa atuyajui kabisa, Hivyo aliwata viongozi hao wa Nssf kuwa nao karibu zaidi ili waweze kubadilisha maisha yao.

Mwenyekiti wa BMU katika mwalo wa Ihale Bw, Pius mazima anasema kuwa sasa ni wakati mwafaka wa wavuvi kujikwamua na kwa hili hata uvuvi harama utakuwa kikomo nchini.


Hakuna maoni :

Chapisha Maoni