Kundi kubwa la watu nchini Ujerumani
wametoa heshima zao za mwisho kwa mwanamke aliyeuwawa wakati
akijaribu kuwazuia mabinti wawili wasidhalilishwe.
Msichana huyo Tugce Albayrak
alifariki dunia Ijumaa baada ya kupigwa kichwani na kupoteza fahamu
nje ya mgahawa wa McDonald karibu na mji wa Frankfurt.
Mamia ya waombolezaji wamehudhuria
ibada ya marehemu iliyofanyika kwenye msikiti mmoja kabla ya mwili
wake kwenda kuzikwa katika mji aliozaliwa.
Mwanaume wa mmoja wa miaka 18
anashikiliwa kutokana na shambulio hilo lililofanyika Novemba 15,
mwaka huu na kuishtua nchi ya Ujerumani.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni