Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani
John Kerry amesema mashambulizi ya anga yaliyoendeshwa na Marekani
pamoja na washirika wake dhidi ya IS yamesababisha madhara makubwa na
kudhoofisha uwezo wa kundi hilo.
Bw. Kerry amesema kampeni dhidi ya
kundi hilo zitachukua miaka mingi, lakini muungano huo utaendelea
kukabiliana na IS kwa muda mrefu zaidi iwezekanavyo.
Mapema Marekani ilisema Iran, ambayo
haipo kwenye muungano imetekeleza mashambulizi ya anga dhidi ya kundi
la IS nchini Irak. Hata hivyo Iran imekanusha taarifa hiyo.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni