.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumanne, 30 Desemba 2014

MSAKO WA NDEGE YA AIRASIA: MIILI 40 YAPATIKANA KATIKA ENEO LA BAHARI


Maafisa wa nchini Indonesia wamepata miili 40 bahari wakati wakitafuta ndege ya AirAsia namba QZ8501, iliyotoweka tangu siku ya jumapili.

Mabaki ya ndege ikiwemo miili hiyo vimeonekana kuelea kwenye bahari ya Java, eneo la kando la Indonesia la Borneo, ambalo ni miongoni mwa maeneo yanayotafutwa ndege hiyo.

Hata hivyo hakuna taarifa rasmi iliyothibitisha miili hiyo imetoka katika ndege hiyo iliyotoweka.

Ndege hiyo aina ya Airbus A320-200, ikiwa na abiria 162 wakitokea Surabaya nchini Indonesia kuelekea Singapore, ilipotea siku ya jumapili.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni