Polisi Hong Kong wamepambana na
wanaharakati wa demokrasia waliojaribu kulizunguka jengo la ofisi za
serikali, katika machafuka mabaya kuwahi kutokea ndani ya miezi
miwili ya maandamano.
Waandamanaji wamepambana na polisi
wenye silaha na mabomu ya machozi ya pilipili katika barabara kwenye
Wilaya ya kiutawala.
Polisi wanasema watu 40 wamekamatwa
pamoja na idadi kadhaa ya maafisa polisi kujeruhiwa katika mapambano
hayo.
Waandamanaji wanataka watu wa Hong
Kong kuruhusiwa kuchagua viongozi wao katika uchaguzi wa mwaka 2017
bila ya kuingiliwa na Beijing.
Polisi akimchapa mjeledi mmoja wa waandamanaji



Hakuna maoni :
Chapisha Maoni