Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani,
Papa Francis, amewasihi viongozi wa Kiislam duniani kulaani vitendo
vya ugaidi vinavyofanywa duniani kwa kutumia jina la Uislam.
Akiongea akiwa kwenye ndege njiani
kuelekea Rome, Papa amesema anatambua namna waislam wema
wanavyoumizwa na watu wanaohusisha Uislam na ugaidi.
Papa Francis alikuwa anarejea nchini
Italia baada ya ziara yake ya siku tatu nchini Uturuki, ambapo
alijadiliana juu ya suala la mgawanyiko baina ya imani.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni