Real Madrid wameshinda kombe lao la
tano kwa mwaka 2014, baada ya kuwafungwa mabingwa wa Amerika ya
Kusini timu ya San Lorenzo na kutwaa Kombe la Dunia kwa vilabu,
katika fainali iliyofanyika Morocco.
Katika mchezo huo mabingwa hao wa
Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya, Mabingwa wa Kombe la Copa del Rey na
Kombe la Super la Ulaya, walipata bao la kuongoza kupitia Sergio
Ramos aliyeutumbukiza mpira kimiani kwa kichwa.
Makosa ya golikipa wa San Lorenzo
yaliiwezesha Real Madrid kupata bao la pili kupitia kwa winga wake
mwenye kasi Gareth Bale, katika michezo huo ambao hadi mwisho matokeo
yalikuwa Real Madrid 2-0 San Lorenzo.
Wachezaji wa Real Madrid wakifurahi ushindi
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni