Mamlaka za Australia zimemfungulia
mashtaka mwanamke mmoja katika mji wa Kaskazini wa Cairns kwa
kuhusika na mauaji ya watoto wake saba pamoja pamoja na mpwa wake.
Polisi wamesema mwanamke huyo
Mersane Warria, 37, amefunguliwa mashtaka hayo akiwa hospitali chini
ya ulinzi baada ya na yeye kujichoma kisu.
Uchunguzi wa kitabibu unafanyika
kubaini chanzo cha vifo vya watoto hao wanane, ambao kati yao wanne
ni kiume na wanne ni wakike wenye umri wa kuanzia miezi 18 hadi miaka
15.
Vilio vikitawala wakati wa kuweka mashada na kuomboleza vifo vya watoto hao
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni