.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 21 Desemba 2014

WALIBERIA WAJITOKEZA KWA WINGI KUPIGA KURA KUWACHAGUA MASENETA

Kura zinaendelea kupigwa katika uchaguzi nchini Liberia ambao ulilazimika kuhairishwa mwezi Oktoba kutokana na mlipuko wa ugonjwa hatari wa Ebola.

Katika uchaguzi huo wananchi wa Liberia wanawachagua wawakilishi wao katika baraza la Seneti.

Miongoni mwa wagombea 139 wanaowania nafasi 15 za Useneta yupo mwanasoka nyota wa zamani wa nchi hiyo George Weah pamoja na Robert Sirleaf, ambaye ni mtoto wa kiume wa rais wa Liberia.

Ugonjwa wa Ebola uliambukiza watu 19,000 katika nchi za Afrika Magharibi na kuuwa watu zaidi ya 7,373, huku vifo 3,346 vikitokea Liberia kwa mujibu wa takwimu za Umoja wa Mataifa.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni