Wanandoa wapatao 2,000 nchini Brazil
wamefunga ndoa katika uwanja wa mpira Jijini Rio de Janeiro, na
kuweka rekodi ya ndoa nyingi kufungwa kwa pamoja katika mji huo.
Ndoa hizo za watu wengi ambazo
hufungwa kila mwaka ambazo zinalenga kusaidia watu wa kipato cha
chini wasiomudu gharama za kulipia kufunga ndoa kuweza kufunga ndoa.
Mamlaka ya Mji wa Rio de Janeiro
inayounga mkono mpango huo, ilikodishwa treni kwa ajili ya
kuwasafirisha wanandoa hao na wageni wao.
Karibu watu 12,000 walihudhuria
sherehe hizo za ndoa za watu wengi zilizofanyika katika uwanja wa
soka wa Maracanazinho arena.


Hakuna maoni :
Chapisha Maoni