Polisi nchini Australia wamesema
watoto wanane wamekutwa wakiwa wamekufa kwenye nyumba huko Cairns
kaskazini mwa Queensland.
Polisi wamesema mwanamke wa umri wa
miaka 34, ambaye ni mama wa watoto wapatao saba amekimbizwa hospitali
akiwa na jeraha la kuchomwa kisu lakini hali yake si mbaya.
Hata hivyo polisi hawajathibitisha
taarifa kuwa watoto hao wenye umri wa kuanzia miezi 18 hadi miaka 15
kama nao wameuwawa kwa kuchomwa visu.
Katika taarifa yake Waziri Mkuu wa
Australia Tony Abbott amesema tukio hilo ni uhalifu usio elezeka.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni