.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumanne, 30 Desemba 2014

YABAINIKA KUWA JUSTIN BIEBER KUMBE HAKUNUNUA NDEGE ANAYOTANUA NAYO

Imebainika kuwa ndege binafsi aliyopiga nayo picha mwanamuziki Justin Bieber, hakuinunua bali ilitolewa kwa ajili ya msanii huyo kutanua nayo wakati wa sikukuu akitokea Canada kuja New York, na ukweli ni kwamba ndege hiyo ipo sokoni.

Msanii Justin Bieber ambaye inaaminika anamali za thamani ya dola milioni 200, itakuwa ni hatari kwake kuinunua ndege hiyo yenye thamani ya dola milioni 60 ikiwa mpya.

Siku ya Alhamisi, mpenzi wake ambaye wamekuwa wakiachana na kurudiana Selena Gomez alijipiga picha akiwa ndani ya ndege hiyo nzuri yenye viti 20 vya abiria, na kisha kutuma kwenye mitandao ya jamii.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni