Mtumishi wa afya ambaye amerejea
kutoka Afrika Magharibi, amebainika kuwa na virusi vya Ebola, na
anapatiwa matibabu katika hospitali Jijini Gasgow.
Mwanamke huyo aliyewasili akitokea
Sierra Leone usiku wa jumapili, amewekwa kwenye chumba cha pekee
kwenye hospitali ya Gartnavel.
Watu wote waliokutana na mtumishi
huyo wanachunguzwa, wakiwemo walikuwa nae kwenye ndege kuja Scotland
hadi Heathrow.
Waziri wa Afya wa Uingereza, Jeremy
Hunt amethibitisha kuwa mtumishi huyo mwanamke atapelekwa katika
kitengo maalum Jijini London.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni