Katika mchezo huo wa kundi B uliokuwa wa kukamilisha ratiba, timu hizo zilitoka uwanjani zikiwa zimefungana bao 1-1.
Tunisia ndio waliokuwa wa kwanza kupata bao lililofungwa katika dakika ya 31 na Ahmed Akaichi, bao ambalo lilidumu hadi kipindi cha kwanza kinamalizika.
Kipindi cha pili Congo walijibu mashambulizi na kufanikiwa kusawazisha bao hilo katika dakika ya 66 mfungaji akiwa ni Bokila.
Kwa matokeo hayo, Tunisia imemaliza wakiwa vinara wa kundi B kwa kuwa na pointi 5 wakifuatiwa na Congo wenye pointi 3. Zote zimesonga mbele hatua ya robo fainali ya michuano hiyo.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni