.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 7 Januari 2015

BOMU LAUWA WATU KADHAA NA KUJERUHI WENGINE NCHINI YEMEN

Makumi ya watu wameuwawa ama kujeruhiwa katika mlipuko nje ya chuo cha polisi katika jiji la Sanaa nchini Yemen.

Taarifa zimeeleza kuwa bomu hilo lilikuwa kwenye gari lililipuliwa karibu na kundi la wanachuo, hata hivyo taarifa hizi bado hazijathibitishwa na mamlaka za nchi hiyo.

Mashahidi wamesema mlipuko huo uliweza kusikika katika eneo kubwa la Jiji la Sanaa, na moshi mkubwa umekuwa ukionekana.

Nchi ya Yemen imeendelea kuwa haijatulia tangu kuibuka maandamano mwaka 2011, yaliyomlazimisha rais aliyekuwa madarakani wakati huo Ali Abdallah Saleh kuachia madaraka.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni