.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Ijumaa, 9 Januari 2015

LIONEL MESSI NA NEYMAR WAREJEA KWA KISHINDO DIMBANI NA KUICHAKAZA ELCHE MABAO 5-0

Wachezaji nyota Lionel Messi na Neymar wamerejea kwa kishindo na kumaliza dhahama za vipigo kwa kuiongoza Barcelona kuichakaza Elche kwa mabao 5-0 katika kombe la Copa del Rey.

Wawili hao walipumzishwa jumapili na kujikuta Barcelona ikipoteza dhidi ya vijana wa kocha David Moyes, Real Sociedad, lakina jana usiku Neymar alikuwa wa kwanza kucheka na nyavu baada ya kupata pande kutoka kwa Luis Suarez.

Katika mchezo huo, Suarez alifunga bao la pili dakika 40 na Messi kuongeza la tatu katika dakika ya 45, Alba naye akafunga dakika ya 56 na Neymar tena akacheka na nyavu dakika ya 59 na kukamilisha karamu ya magoli.
                                                                 Neymar akimchambua kipa wa Elche
                                                                             Suarez akijipinda kufunga bao 
                                                         Lionel Messi akifunga kwa shuti la penati

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni