.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 11 Januari 2015

MABAKI YA NDEGE YOTE YA AIRASIA YAAMINIKA KUWA YAMEBAINIKA CHINI YA BAHARI

Timu inayotafuta ndege ya Indonesia inaamini kuwa imebaini yalipo mabaki yote ya ndege ya AirAsia namba QZ8501.

Maafisa wameeleza kuwa umbo la kitu kama ndege limebainika baada ya kutumia kipimo cha sonar scan katika eneo ambalo zoezi la kuitafuta ndege hiyo katika bahari ya Java linaendelea.

Maafisa hao wanamatumaini sanduku la "black box" linalorekodi mawasiliano na taarifa nyingine za ndege litakuwepo karibu na umbo lililobainika karibu na eneo ambalo mkia wa ndege hiyo ulipatikana.

Ndege hiyo ilitoweka na kupoteza mawasiliano ikiwa na abiria 162, ikitokea Surabaya nchini Indonesia kwenda Desemba 28 kutokana na hali mbaya ya hewa.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni