.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Ijumaa, 2 Januari 2015

MAHAKAMA KUU KENYA YASITISHA VIFUNGU KADHAA VYA SHERIA TATA YA USALAMA

Mahakama Kuu ya Kenya leo imesitisha kwa muda utekelezaji wa baadhi ya vifungu vya sheria yenye utata ya usalama, wakati ikingojea usikilizaji wa kesi ya msingi iliyofunguliwa na muungano wa Cord kuipinga sheria hiyo.

Miongoni mwa vifungu vya sheria vilivyositishwa kutumika ni pamoja na kifungu namba 12, 29, 48, 56, 58, na 58. Katika uamuzi wake Jaji Justice George Odunga amesema baadhi ya vifungu vinakiuka haki za msingi.

Kiongozi wa muungano wa Cord Raila Odinga amepokea kwa furaha uamuzi huo wa Mahakama Kuu, na kusema kupitia mahakama imeweza kulinda haki za watu.
Kiongozi wa Cord Bw. Raila Odinga kati kati akinyanyua mkono juu kufurahia uamuzi wa mahakama

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni