Miili minne zaidi ya watu
imepatikana katika bahari ya Java wakati wa zoezi la kutafuta mabaki
ya ndege ya AirAsia namba QZ8501 likiingia wiki ya pili.
Mkuu wa timu inayoendesha zoezi la
kuitafuta ndege hiyo Bambang Soelistyo amesema hadi sasa miili 34
imepatikana ikiwemo na mabaki matano ya vipande vya ndege hiyo.
Hata hivyo hali mbaya ya hewa
imewalazimisha wazamiaji kusitisha jaribio la kuifikia ndege hiyo
kwenye eneo la chini ya bahari ambapo miili mingi ya watu inaaminika
imekwama. Ndege hiyo ilianguka ikiwa na abiria 162.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni