Mtoto mchanga wa kike mwenye asili
ya Roma, amenyimwa eneo la kuzikiwa na meya mmoja nchini Ufaransa, na
kupelekea kuibuka kwa malalamiko kutoka kwa kundi la wanaharakati wa
haki za binadamu.
Mtoto huyo aliyefariki dunia siku ya
Krismasi, kwa kifo kilichotokana na maradhi yanayowaandama watoto
wachanga, amenyimwa eneo la kuzikwa huko Champlan, kusini mwa Jiji la
Paris.
Meya wa Champlan amesema kipaumbele
cha eneo la kuzikia anatoa kwa walipa kodi tu, hata hivyo Meya wa
eneo la jirani la Wissous, Richard Trinquier amekubali kutoa eneo la
kumzika mtoto huyo na kusema uamuzi wa meya mwenzake ni wa ajabu.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni