.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 4 Januari 2015

KOREA KASKAZINI YADIA VIKWAZO ILIVYOWEKEWA NI SERA ZA UHASAMA ZA MAREKANI

Korea Kaskazini imeelezea vikwazo vipya ilivyowekewa kutokana na kushambulia wavuti ya kampuni ya filamu ya Sony, kuwa havina sababu yoyote na ni sera za uhasama za Marekani.

Marekani imeziwekea vikwazo taasisi za Korea Kaskazini pamoja na watu binafsi 10, baada ya Shirika lake la Ujasusi la FBI, kuilaumu serikali ya Pyongyang kwa kushambulia wavuti ya Sony.

Korea Kaskazini imekanusha kuhusika na tukio hilo, hata hivyo ilipongeza kitendo hicho cha kushambuliwa kampuni ya Sony.

Tukio hilo lilitokea wakati kampuni Sony ikiwa inakaribia kutoa filamu ya The Interview, ambayo inaelezea jaribio la kutaka kumuua kiongozi wa Korea Kaskazini.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni