.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 4 Januari 2015

ZOEZI LA KUTAFUTA MABAKI YA NDEGE YA AIRASIA LAINGIA WIKI YA PILI

Zoezi la kutafuta mabaki ya ndege ya AirAsia namba QZ8501 katika bahari ya Java linaingia katika wiki ya pili, huku hali mbaya ya hewa ikikwamisha operesheni hiyo.

Wazamiaji wanatarajia kubadilikka kwa hali ya hewa na kuwa nzuri, hata hivyo bado wanalazimika kuchukua tahadhari kwa sasa.

Kitu kikubwa cha tano kinachozaniwa kuwa ni mabaki ya ndege hiyo, kimeonekana chini ya bahari, na mwili mmoja umepatikana na kufanya idadi ya miili iliyopatikana kufikia 31.

Ndege hiyo ilianguka baharini ikitokea Surabaya nchini Indonesia kwenda Singapore jumapili ya wiki iliyopita ikiwa na watu 162.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni