Mtoto mwenye asili ya Roma atazikwa
kwenye makaburi Ufaransa baadae, huku kukiwa na mgogoro kuhusiana na
taarifa za meya wa mji karibu na alipofariki mtoto huyo wa kike
kugoma kutoa eneo la kuzikia.
Mtoto huyo atazikwa huko Wissous,
kusini mwa Paris baada ya mji wa Champlan kuripotiwa kuinyima familia
yake eneo la kumzika, hata hivyo meya wa mji huo jana alikanusha
madai hayo baada ya kuibua shutuma za wananchi.
Waziri Mkuu wa Ufaransa, amekiita
kitendo hicho kuwa ni sawa na tusi kwa Ufaransa, na afisa wa nchi
hiyo anayehusika na kulinda haki za binadamu ametangaza kuanza kwa
uchuguzi wa tukio hilo.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni