Kocha aliyetimuliwa Manchester
United, David Moyes, ameiongoza timu yake mpya ya Real Sociedad kuipa
kipigo Barcelona na kutinga nafasi za juu za msimamo wa ligi ya La
Liga baada ya kupata ushindi wa bao 1-0, pongeze zikienda kwa
mchezaji wao Jordi Alba.
Huku Real Madrid ikiwa imelala 2-1
dhidi ya Valencia katika mchezo wa awali, ilikuwa fursa kwa timu hiyo
ya Barcelona maarufu kama the Catalans kukwea juu ya msimamo wa ligi
na kuongeza ushindani wa kuwani kutwaa ubingwa.
Katika mchezo huo kocha Luis Enrique
aliwaanzisha benchi wachezaji wake Lionel Messi, Neymar pamoja na
Dani Alves, kutokana na kuwa walikuwa kwenye mapumziko, lakini hata
alipowaingiza baadae hawakufanikisha kubadili matoke.
Neymar akizuiwa kukatiza kwenda kufunga goli
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni