.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 5 Januari 2015

NAIBU WAZIRI WA MAJI, MH MAKALLA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA JIJINI DAR, AKAMATA WEZI WA MAJI NA KUAGIZA BAADHI YA WATENDAJI WA DAWASCO WATIMULIWE KWA UZEMBE


Naibu Waziri wa Maji, Mh Amos Makalla amefanya ziara ya kushtukiza katika mkoa wa Dar es salaam, ambapo katika ziara hiyo amefanikiwa kukamata wezi wa maji 12. Pia Mh Makalla awatimua mameneja wa maji wa Boko na kimara kutokana na utendaji wao mbovu. Katika ziara hiyo ya ghafla, Mh Mkalla ametangaza operasheni kubwa zaidi kusaka wezi wa maji. Hapa Naibu Waziri huyo wa Maji akiongea na wananchi wa Boko.
Naibu Waziri wa Maji, Mh Amos Makalla ( mwenye shati la kitenge ) akiwa katika ziara ya ghafla jijini Dar es Salaam kukagua miundombinu ya maji maeno ya Boko, ambapo pia amekamata wezi wa maji waliojiunganishia kinyemelea.
Mh Makalla akimsikiliza mmoja wa wananchi waliojitokeza kutoa maoni yao wakati waziri huyo aipokuwa katika ziara ya kukagua miundombinu ya maji maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam. Hapa ilikuwa maeneo ya Manzese
Ziara imepamba moto kuhakikisha wananchi wa jiji wanapata maji na kuwakamata wanaohujumu miundombinu ya maji.

Naibu Waziri wa Maji, Mh Amos Makalla akiangalia jinsi maji yanavyoibiwa maeneo ya Magomeni.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni