.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Ijumaa, 9 Januari 2015

POLISI NCHINI UFARANSA WAZINGIRA JENGO WALIOMO WATUHUMIWA WA MAUAJI YA WATU 12 JIJINI PARIS

Polisi nchini Ufaransa wamelizingira jengo moja katika mji wa kaskazini, ambalo watu wawili wanaotuhumiwa kuhusika mauaji katika ofisi za jarida la vibonzo la Charlie Hebdo, wanadaiwa kuwamo.

Milio ya risasi imesikika na watu kadhaa inasemekana wamejeruhiwa katika eneo la Dammartin-en-Goele, lililopo kilomita 35 kutoka Jiji la Paris.

Hatua hiyo imefikiwa ikiwa karibu saa 48 kupita tangu kutokea shambulio katika ofisi za jarida la vibonzo la Charlie Hebdo na kuuwa watu 12.
                                                     Polisi wakikimbilia kulizingira jengo hilo
                                           Uangalizi hadi angani kuhakikisha hatoki mtu

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni