Maafisa wa Marekani wamesema jeshi
la polisi limekagua ndege mbili katika uwanja wa Atlanta, baada ya
kupatiwa taarifa za uhakika za tishio la kuwepo bomu.
Msemaji wa uwanja huo Reese McCranie
tishio hilo lilitolewa kwa ndege za mashrika ya ndege ya Delta na
Southwest zinazotoka Potland na Milwaukee.
Amesema kuwa baada ya taarifa hizo
ndege za shirika hilo zimetua salama katika uwanja wa ndege wa
kimataifa wa Hartsfield-Jackson.
Ndege mbili za kivita za Marekani
zilizisindikiza ndege hizo katika uwanja wa Hartsfield-Jackson na
baadae kuelezwa kuwa hakuna bomu lililokutwa.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni