Waziri wa Ulinzi wa Zambia Edger
Lungu wa Chama cha Patriotic Front ameshinda nafasi ya urais katika
uchaguzi uliofanyika siku ya jumanne.
Lungu ameshinda kwa kura 48.3, tume
ya uchaguzi imetangaza, katika uchaguzi huo ambao matokeo yake
yamechelewa kutolewa.
Mpinzani wake Hakainde Hichilema wa
chama cha United Party for National Development, ambaye mapema
alitangaza kuukosoa uchaguzi huo kwa kuvurundwa amepata kura 46.7.
Uchaguzi huo wa urais Zambia
uliitishwa kutokana na kifo cha rais Michael Sata kilichotokea mwezi
Oktoba mwaka jana.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni